+10 344 123 64 77

Monday, July 20, 2015

WIVU WA MAPENZI NDO UMMENIFANYA HIVI.......FUATILIA HAPA TUKIO KAMILI

christy
Christy Sims ni mwanadada ambaye maisha yake yalibadilika ghafla baada ya aliekuwa mpenzi wake wa muda mrefu kumuachia majeraha ambayo hatokuja kuyasahau maishani.
Akiwa na miaka 40 Christy amelazimika kuishi na makovu baada ya kumwagiwa tindikali  na ex-boyfriend wake kwa sababu tu ya wivu wa mapenzi, kumhisi kuwa anatembea na mtu mwengine.
christy2
Christy Sims kabla ya tukio la kumwagiwa tindikali.
Haya yote yalitokea weekend moja ya mwaka 2013 nyumbani kwa mpenzi wake ambaye aliamua kumwagia dada huyu tindikali usoni, kifuani na mikononi kitendo kilichosukumwa na hasira kali za wivu.
Christy alipiga kelele nyingi na kuomba msaada lakini boyfriend wake aliamua kumuacha aungue mpaka watu wa huduma ya kwanza walipofika na kushangazwa kwa nini boyfriend huyo hakuchukua hatua za  kumpatia girllfriend wake huduma ya kwanza.
christy4
Christy Sims sasa hivi analazimika kuvaa miwani ya jua kila muda kulinda macho yake yasipigwe na jua la kumuumiza.

0 comments:

Post a Comment