+10 344 123 64 77

Monday, November 2, 2015

JB:: SIPENDI USHABIKI USUI WA MAANA!!!!!.....UPI HUO??? BOFYA HAPA KUTAZAMA

JB: Sitaki Watu Wenye Ushabiki wa Kijinga…
ni Staa wa bongo Movies, Jacob Stephen ‘JB’ ambaye alikuwa ni moja ya wasanii wa bongo movies ambao walikuwa wakikipigia kampeni chama cha mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi uliyopita, amewafungukia baadhi ya mashabiki kwenye ukurasa wake wa Instagram ambao wamekuwa wakiendeleza siasa hadi kwenye kazi yake ya sanaa.
Narudia kwa mara ya mwisho kwenye acc yangu sitaki watu wenye ushabiki wa kijinga....sitaki matusi...hivi unaposema tutaburn cd hatununui tena unafikiri unanikomoa mimi peke yangu...zile library na maduka ya CD zote za wana CCM????hii ni tasnia walianza akina marehemu Mzee Jongo,Small na wengine mpaka ikafika kwetu nani anajua baada ya sisi pengine atakuja mwanao...Baba yake Sharukh Khan hakujua kama baada ya Mithun atakuja mwanae...mbona sisi tunashirikiana na wasanii wa UKAWA.
Acheni kuchochea ujinga lakini sishangai hata kiongozi mmoja wa ukawa alidiriki kusema watu wasinunue bidhaa za asas kule iringa...kisa mmiliki ni CCM..wakati tunalilia viwanda wanaofaidikiwa ni CCM peke yao????? sijui mnaipeleka wapi hii nchi...Sitaki ujinga huu kwemye acc yangu +255 kwanza
JB aliandika hayo mara nbaada ya kuweka picha hiyo hapo juu akiwa na Shamsa Ford ambaye ni mwana UKAWA.

0 comments:

Post a Comment