+10 344 123 64 77

Thursday, May 7, 2015

DAH!!!! HUU SASA NI UKATILI UMEPITILIZA======>>soma kisa hapa

 
Halima anayedaiwa kumwagiwa maji ya moto.
Kwa mujibu wa chanzo ambacho ni ndugu wa majeruhi huyo, tukio hilo lilijiri mwezi uliopita ndani ya baa moja maarufu iliyopo maeneo ya Ubungo, Dar es Salaam ambapo majeruhi huyo anafanyia kazi baada ya mwanamke huyo kuamini Halima anatembea na mtalaka wake.
Inadaiwa kuwa, mwanamke huyo ambaye ni mtuhumiwa na mwanaume mmiliki wa baa aliyejulikana kwa jina moja la Mushi waliachana miaka mingi iliyopita.“Lakini mwanamke akawa anamfuatilia mumewe kila siku na kwa kila kitu. Ilifika mahali akaambiwa kuwa, mwanaume huyo aliyetengana naye ana uhusiano wa kamapenzi na baamedi wake mmoja.”
“Ndipo siku ya tukio, mwanamke huyo alifika kwenye baa hiyo akitoka kusikojulikana. Wakati huo, Halima alikaa kwenye kiti akiangalia kaunta. Mwanamke huyo alipitiliza jikoni, akachukua sufuria yenye maji ya moto akammwagia Halima bila kujua kuwa, siye aliyemlenga mpaka Halima aliposema ‘siyo mimi’.”
Jeraha alilolipata sehemu ya bega.
“Ni ukatili mkubwa sana kutendeka maana hakuna ukweli wowote kwamba, yule baamedi alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na bosi wake na hakulengwa yeye. Halafu hata kama ni kweli alikuwa na uhusiano naye, yeye walishaachana kwa miaka saba nyuma, sasa wivu wa nini?” kilisema na kuhoji chanzo hicho.
“Ishu ilikwenda kisheria kabisa, walikubaliana kuachana. Wakagawana mali na hata watoto waligawana. Wapo watoto wanne, mwanamke akachukua wawili, wengine wakabaki kwa baba yao.Kikaendelea: “Mbaya zaidi, baada ya ukatili huo, yule mtuhumiwa hakuchukuliwa hatua zozote zile! Hii inaonesha ni jinsi gani wanyonge wanaishi kwa hatari ndani ya nchi yao wenyewe. Pale hakuna cha bahati mbaya bwana.
“Halima hakuwa na pesa za kujitibu zaidi ya kutegemea misaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walifahamu kisa kizima. Inauma sana kwa kweli.”Baadhi ya vyanzo vilidai kwamba, baada ya tukio hilo, mtuhu

0 comments:

Post a Comment