+10 344 123 64 77

Sunday, May 24, 2015

JENGUA!!! UKATILI WANGU KATIKA SANAA NDO UMENIFANYA NIWE HAPA SASA

Ukatili Wampa Ulaji Jengua

 
 NI Muigizaji mkongwe wa hapa Bongo YETU, Mzee Jengua  amesema kuwa ameshirikishwa  katika filamu ya Sio Dili inayohusu mauaji ya Albino kutokana na hulka yake ya ukatili awapo kazini.
Akizungumza na Gazeti la Nipashe , Jengua  alisema  muandaaji wa filamu hiyo aliona yeye ndio  anafaa kuwa mtu  anayefanya biashara ya viungo vya Albino kutokana na uigizaji wake wa ukatili, katika filamu zilizopita.
Jengua hata hivyo amesema anaumizwa na tabia za watu ambao hukata viungo vya au kuwaua  kwa imani za kishirikina .
“Filamu ya Sio Dili  ni harakati ya kupambana  na mauaji ya Albina na itakuwa elimu kwa watanzania wote alisema Jengua.

0 comments:

Post a Comment