Home
/ Hakuna wa kufanana na Ngwea bongo – TID......
Sunday, May 29, 2016
Hakuna wa kufanana na Ngwea bongo – TID......
Msanii TID amesema mpaka sasa kwenye maisha yake ya muziki hajawahi kuona msanii ambaye atachukua kiti cha aliyekuwa mkali wa ‘free style’ bongo, Albert Mangwea, aliyefariki miaka mitatu iliyopita.
Akijibu swali la mtangazaji wa kipindi cha Friday Night Live Sam Misago, alipomuuliza iwapo kuna msanii yeyote anayefikia uwezo wa Ngwea, TID alisema mpaka sasa hakuna wa kuweza kumfananisha na Ngwea.
‘What are u saying…! Ngwea!? Hakuna msanii anayeweza kumfikia Ngwea, that man was special, Ngwea alikuwa blessed! Alafu umfananishe na nani…Bill Nas anaweza kuwa a half of it lakini hawezi kuwa kama Ngwea, Ngwea can rap, Ngwea can sing, Ngwea can give u a melody..alafu umfananishe na mtu, hakuna wa kufanana naye, no one!”, alisikika TID akijibu.
Pamoja na hayo TID amesema yeye kama rafiki yake ataendelea kuenzi kazi zake, na amewashukuru wasanii waliojitokeza kufanya show ya kumbukumbu yake, na kuweza kumsaidia mama mzazi wa Albert Mangwea ikiwa kama kumuonyesha kuwa walikuwa wanampenda mtoto wake.
bongomove
Surya
Out too the been like hard off. Improve enquire welcome own beloved matters her. As insipidity so mr unsatiable increasing attachment motionless cultivated. Addition mr husbands unpacked occasion he.
0 comments:
Post a Comment