+10 344 123 64 77

Wednesday, August 12, 2015

KABULA MAARUFU KWA JINA LA JINI KABULA AMSHANGAA BUSHOKE.....FUATILIA HAPA



 maarufu kama Jini Kabula, NI MIRIAM Jolwa, ambaye ni staa kutoka Bongo Movie, amemshangaa aliyekuwa mpenzi wake, Ruta Bushoke kumkana kuwa hawajawahi kuwa wapenzi.
Akistorisha na gazeti hili hivi karibuni, Kabula alisema maneno ya mkali huyo wa muziki wa Kizazi Kipya yanaashiria kama mtu anayechanganyikiwa, kwani asingeweza kujinadi kuwa ni mpenziwe kama haikuwa hivyo.
“Yaani inawezekana Bushoke anataka kupata uchizi kwa kweli, hivi kuna mtu anaweza kujinadi kuwa ni mpenzi wa mtu wakati siyo! Kwanza kwa kitu gani jamani? Nina  wasiwasi naye kwamba siyo mzima,” alisema Kabula.
Wiki chache zilizopita, Bushoke aliyeimba kibao  cha Mume Bwege, aliwahi kudai kuwa hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Jini Kabula.

0 comments:

Post a Comment