+10 344 123 64 77

Tuesday, May 10, 2016

SIWEZI KUMUHUKUMU NAY.....SHAMSA

STAA wa Bongo Muvi, Shamsa Ford kwa mara ya kwanza ameibuka na kuiongelea Ngoma ya Shika Adabu Yako iliyoimbwa na Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kuwa kamwe hawezi kumhukumu Nay kwa maneno aliyoimba.
SHAMSA21
“Namuacha kama alivyo na kamwe siwezi kumhukumu kwa kile alichokiimba labda kwa upande wake aliona ni sawa,” alisema Shamsa.
Katika Wimbo wa Shika Adabu Yako, Nay amewachana mastaa wa Muziki na Bongo Muvi ambao ni Shetta, Ommy Dimpoz, Ray, Niva, Wema Sepetu na wengine wengi jambo lililosababisha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kuufungia wimbo huo kutokana na ukiukwaji mkubwa wa maadili, kashfa, uchochezi na kudhalilisha watu.

0 comments:

Post a Comment