+10 344 123 64 77

Thursday, May 28, 2015

DAH!!!! IVI NI KWELI MTOTO WA ANTI EZEKIEL APIGWA ZENGWE???? HEBU TUANGALIE HAPA


Mtoto wa kike wa staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson aliyejifungua mwishoni mwa wiki iliyopita na kumpa jina la Cookie (keki ndogo lakini tamu) anaanza kung’aa kwenye vyombo vya habari baada ya baadhi ya watu kumpiga zengwe la madai kwamba eti hafanani na baba yake, Moses Iyobo ‘Moze’.

 ni ==>> Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson.
Huku ishu hiyo ikipingwa vikali na Aunt, washakunaku wa mambo ya watu waliozungumza na Amani  baada ya kumuona Cookie walidai kwamba mtoto ni mweupe wakati Moze ni mweusi ‘tiii’.Zengwe hilo lilianza kusambaa miongoni mwa mashosti waliokwenda kumpa hongera Aunt nyumbani kwake, Kinondoni, Dar, saa chache baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.
>>>Unajua tangu akiwa mjamzito kuna watu walikuwa na shauku ya kumuona mtoto kujua kama kweli ni wa Moze maana mwanzoni hakuna aliyeamini kama mimba ni ya Moze ‘s0’ hao ndiyo wameanza chokochoko,” kilisema chanzo chetu kwa sharti la kutochorwa gazetini.


0 comments:

Post a Comment