+10 344 123 64 77

Monday, May 11, 2015

HABARI!!! MGANGA WA JADI AKUTWA AKIFANYA HAYA HUKO MARA====>>soma zaidi

MGANGA mmoja wa kienyeji amekamatwa akifanya ushirikina katika Mahakama ya wilaya ya Bunda mkoani Mara kwa kutumia tunguli ili kuwezesha kushinda kesi  hiyo.

Mganga huyo ni moja kati ya waganga sita, ambao walikamatwa kwa kosa la kupiga ramli chonganishi na kufunguliwa kesi katika mahakama hiyo ya wilaya mkoani hapo.

Mtuhumiwa huyo pamoja na wenzake hao, walikamatwa Machi 11 mwaka huu saa 6:00 mchana katika kijiji cha Kabasa wilayani hapa, wakipiga ramli chonganishi ya kuchonganisha wananchi kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa huyo aliyeshikwa juzi akifanya ushirikina huo katika mahakama hiyo ni Riku Wasaga Yahaya (50), mkazi wa kijiji cha Kabasa wilayani hapa.

Mtuhumiwa huyo pamoja na wenzake hao, walipokamatwa wakipiga ramli chonganishi, walifunguliwa kesi namba 86 ya mwaka huu katika mahakama hiyo
.

0 comments:

Post a Comment